Skip to main content

Watanzania Wamlilia Maximo

Marcio Barcellos Maximo alimaliza mkataba wake wa kuinoa Taifa stars (Timu ya soka ya taifa ya Tanzania) mwaka 2010 mwezi wa saba, baada ya kuinoa timu hiyo kwa mafanikio kwa muda wa miaka minne. Kati ya mafanikio yaliyoletwa katika soka la Tanzania na mbrazili huyu ni pamoja na kurudisha mapenzi ya wapenzi wa mpira kwa timu yao ya Taifa.

Haikuwa kazi ndogo hata kidogo kwa mbrazili huyu kuifanya timu hii iwe kipenzi tena cha watanzania, ni juhudi ya hali ya juu iliyopelekea imani ya watanzania kwa timu yao kurejea tena. Na hii ilitokana na ukweli kuwa Taifa stars ikaanza kuwa mpinzani wa kweli mara inapokutana na timu mbalimbali za bara la Africa.

Misingi mikuu ya filosofia ya mwalimu huyu ilikuwa katika kujenga nidhamu ndani ya timu, umuhimu wa wachezaji kuthamini kazi yao hii ikiwa ni pamoja na kuzingatia mazoezi, umuhimu wa kujenga timu ya muda mrefu. Katika kuyafanikisha haya yote Maximo aliweza si tu kwa timu yake kuonyesha mchezo mzuri uwanjani bali pia aliweza kuwatumia vijana wadogo chipukizi kama Jerryson Tegete kwa mafanikio.

Ule msemo usemao usione vyaelea vimeundwa ukawapitia mbali kidogo watanzania na kuona alichofanya Maximo ni kidogo, na wao wanaweza kufanya zaidi. Mashabiki na baadhi ya vyombo vya habari vilivyoibuka na dhana ya uchambuzi wa soka vikaanza kumsakama kocha huyu. Tuhuma za kutokuona mchango wa kocha zikaanza kuvuma kila pembe ya nchi, majina ya baadhi ya makocha wazawa yakaanza kutajwa huku na kule kuwa wanauwezo mkubwa kuliko mbrazili huyu. Visa vikaanza kuingia hadi kwa wachezaji, wachezaji wenye kuonyesha nidhamu mbovu wakakingiwa kifua na watanzania, kana kwamba Maximo anawaonea. Na baadhi ya wachezaji hao wameshindikana hadi leo.

Mengi yamefanywa na kocha huyu ikiwa ni pamoja nakupanda kwa timu yetu katika chati za FIFA, Kuweza kushiriki michuano ya kimataifa ya Africa kwa wachezaji wa ndani. Haya yote hayakutosha watu wakataka aondoke na yeye kweli akaondoka. Leo katika pita pita yangu katika mitandao nimekutana na discussion katika jamii forum, cha kushangaza ni kuwa wachangiaji karibu wote wanalalamika kuwa kuondoka kwa Maximo ilikuwa ni kosa kubwa sana kwa soka la Tanzania. Jionee mwenyewe katika link hii http://www.jamiiforums.com/sports/215516-namkumbuka-sana-marcio-maximo.html

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Mimi na marafiki

Picha hii ilipigwa pale uwanja wa bandari Tandika nikiwa na wakongwe James Kisaka(aliyesimama kushoto ) na Seifdin Kabange (Jezi nyekundu na white strips). Hii ilikuwa baada ya mazoezi ya Veterans wa NBC United

Dar Young Africans Vs Simba Sports club

Tommorow (saturday 31/10/2009) is one of the big days in Tanzanian Soccer. Tanzania's soccer giants Yanga (young Africans) and Simba will clash at the National stadium in Dar es Salaam. The match is expected to attract many spectators than usual, we expect revenue collections to be high. Actually we look forward to watching this big event. In the midst of expectation I can not stop myself from wondering what actually will happen tommorow. I wish to very advanced soccer tactics from the big teams, I wish to hear from TFF that they have collected as much as they expected as gate collection, I wish to see fair officiating of the match. I wish to mature and fair behavior from fans, i wish for a lot good things to happen. But I know one thing for sure: It is possible that I wont see any of my wishes coming true. It is possible to hear from TFF saying that they run deficit from the match collection. We may end up seeing the usual none fair play game from players, players from each team m...

PURPOSE OF DIFFERENT TACTICAL EXERCISES IN SOCCER

Dear readers I would like to take this opportunity to appologize for not updating information on this site for such long time. Today I just want to highlight purposes for some tactical exercises 2v1 ONE ACTS, ONE SUPPORTS, IN ATTACK OR WHEN DEFENDING. IN ATTACK, PLAYER WITH THE BALL COMMITS THE LONE DEFENDER THEN EITHER GOES PAST THEM OR PASSES TO THE SECOND ATTACKER. IN DEFENSE, NEAREST CHALLENGES, THE OTHER COVERS 3v1 IN DEFENSE, ONE CHALLENGES, ONE COVERS, THE THIRD BALANCES IN ATTACK, ONE COMMITS AN OPPONENT, ONE POSITIONS TO RECIEVE A POSSIBLE PASS, THE THIRD MAKES AN ATTACK RUN 4v2 DEFENDING - IS ABOUT THE 2 WORKING AS A PAIR TO CUT DOWN QUICKLY ANY POSSIBLE EASY SPACE FOR THE OPPONENT WITH THE BALL TO PASS TO ONE OF THE OTHER THREE ATTACKERS ATTACKING - IS ABOUT THE PLAYER WITH THE BALL HAVING THREE OPTIONS TO PASS IF THEY WISH TO (SUPPORT, PASS OPTIONS) 5v2 AS c. ONLY DEFENDING BECOMES MORE OF A POSITIONING TO FORCE THE BALL TO WHERE YOU CAN ATTACK IT FOT ATTACKING ITS ABOU...