Kwa muda mrefu sasa tumekuwa tukisikia malalamiko juu ya Kocha Marcio Maximo wa Taifa Stars, malalamiko haya yamekuwa yakiongezeka kutokana na baadhi ya makocha maarufu wa kitanzania nao kuchochea kelele hizi.
Maximo amekuwa akilalamikiwa sana kwa mambo makuu mawili kwa sasa;
1. Kumuacha Golikipa Juma Kaseja Juma
2. Kuwaacha Athman Idd na Haruna Moshi
Limeongezeka jingine la kuwa kamuita kipa namba mbili wa stars katika kikosi cha Taifa.
Naomba kwa upeo wangu mdogo niyaongelee haya matatu.
1. Sidhani kama tiba ya Stars ni Juma Kaseja golini; Juma Kaseja sio Kipa mzuri kiasi hicho inavyodhaniwa. Ninachoweza kusema kwa sasa ni kuwa nyota ya Juma Kaseja inang'aa machoni kwa watanzania na si kwamba ana kiwango kikubwa sana golini. Wanasimba wanasahau kama kuna kipindi walikuwa hamtaki kipa huyu kwa sababu ya kufungwa na huku wakisema yeye ndio chanzo. Simba wanasahau jinsi alivyokuwa akifungwa katika mashindano ya Tusker mwaka ule Kagera sugar ilipoivua Simba ubingwa huo.
Juma Kaseja amekuwa kipa namba moja ya timu ya taifa kuliko makipa wote wanaocheza sasa,kipindi chote hicho ameisaidaje stars? Watanzania wanakumbuka mashindano ya Kagame yaliaofanyika hapa mwaka juzi? Watanzania wanakumbuka jinsi alivyokuwa akifungwa na Mbui Twite? Wanaomlilia Kaseja kuwa ndio kipa bora Tanzania, wamemuona Amani Simba awapo golini? Si kweli kuwa Kaseja ndio tiba ya matatizo ya Tanzania katika soka tuangalie tatizo halisi,na sio kwa kutafuta shortcut. Tatizo letu kubwa lipo katika kukuza vipaji vya magolikipa.
Nenda katika timu yoyote uone kama makipa wanafundishwa ipasavyo; walimu wengi hawatilii mkazo program za magolikipa katika timu zao. sio ajabu kukuta makipa wa timu wakifanya mazoezi peke yao bila mwalimu. Mwalimu anakuwa busy na program zingine za timu kama ufungaji, viungo nk.
2. Hili la akina Athman Idd na Haruna Moshi nalo la kulipigia kelele. Kuna asiyejua nidhamu za wachezaji hawa? Au ndio yale mambo ya mzazi kukana kwa kusema mwanangu sio mwizi ilhali wajua fika tabia ya mwanao. Ni mara ngapi wachezaji hawa wameadhibiwa na vilabu vyao, TFF? na hakuna aliyepiga kelele. Leo wanaadhibiwa na Maximo watu wanakuja juu, au kocha mgeni hana haki ya kuadhibu mchezaji wa Tanzania?Tunafuga ubovu ambao hautusaidii kabisa.
Labda nimalizie kwa kuwakumbusha Makocha wazalendo maamuzi yao waliyoyafanya hapo nyuma ambayo hayana tofauti sana na kile anachofanya Maximo kwa sasa.
S.Mziray: Kocha huyu wakati akiwa kocha mkuu wa timu ya taifa aliwahi kumuita kikosini mchezaji Magadula ambaye alikuwa hajawai kucheza super ligi hata mara moja.
Sunday Kayuni: Aliwahi kumuita kikosini mchezaji Nteze John Lungu ilhali machezaji huyu alikuwa akisotea benchi katika timumyake ya Simba.
Wito wangu kwenu nyote ni kuwa hatuisaidii timu ya taifa kwa kupiga kelele zisizo na msingi, tutambue ukweli tufanye kazi kulekebisha matatizo yaliyopo katika taifa. Sio lazima wote tuwe makocha wa timu ya Taifa, tunaweza kutoa mchango kwa Taifa kwa kulea vipaji hata katika maeneo tunayoishi.
Mbona sijaona kampeni za watu kumpongeza Maximo pale timu inapofanya vizuri? Ina maana toka apewe timu hajawahi kufanikiwa? au tunafumbia macho mafanikio na kuangalia matatizo?
Maximo amekuwa akilalamikiwa sana kwa mambo makuu mawili kwa sasa;
1. Kumuacha Golikipa Juma Kaseja Juma
2. Kuwaacha Athman Idd na Haruna Moshi
Limeongezeka jingine la kuwa kamuita kipa namba mbili wa stars katika kikosi cha Taifa.
Naomba kwa upeo wangu mdogo niyaongelee haya matatu.
1. Sidhani kama tiba ya Stars ni Juma Kaseja golini; Juma Kaseja sio Kipa mzuri kiasi hicho inavyodhaniwa. Ninachoweza kusema kwa sasa ni kuwa nyota ya Juma Kaseja inang'aa machoni kwa watanzania na si kwamba ana kiwango kikubwa sana golini. Wanasimba wanasahau kama kuna kipindi walikuwa hamtaki kipa huyu kwa sababu ya kufungwa na huku wakisema yeye ndio chanzo. Simba wanasahau jinsi alivyokuwa akifungwa katika mashindano ya Tusker mwaka ule Kagera sugar ilipoivua Simba ubingwa huo.
Juma Kaseja amekuwa kipa namba moja ya timu ya taifa kuliko makipa wote wanaocheza sasa,kipindi chote hicho ameisaidaje stars? Watanzania wanakumbuka mashindano ya Kagame yaliaofanyika hapa mwaka juzi? Watanzania wanakumbuka jinsi alivyokuwa akifungwa na Mbui Twite? Wanaomlilia Kaseja kuwa ndio kipa bora Tanzania, wamemuona Amani Simba awapo golini? Si kweli kuwa Kaseja ndio tiba ya matatizo ya Tanzania katika soka tuangalie tatizo halisi,na sio kwa kutafuta shortcut. Tatizo letu kubwa lipo katika kukuza vipaji vya magolikipa.
Nenda katika timu yoyote uone kama makipa wanafundishwa ipasavyo; walimu wengi hawatilii mkazo program za magolikipa katika timu zao. sio ajabu kukuta makipa wa timu wakifanya mazoezi peke yao bila mwalimu. Mwalimu anakuwa busy na program zingine za timu kama ufungaji, viungo nk.
2. Hili la akina Athman Idd na Haruna Moshi nalo la kulipigia kelele. Kuna asiyejua nidhamu za wachezaji hawa? Au ndio yale mambo ya mzazi kukana kwa kusema mwanangu sio mwizi ilhali wajua fika tabia ya mwanao. Ni mara ngapi wachezaji hawa wameadhibiwa na vilabu vyao, TFF? na hakuna aliyepiga kelele. Leo wanaadhibiwa na Maximo watu wanakuja juu, au kocha mgeni hana haki ya kuadhibu mchezaji wa Tanzania?Tunafuga ubovu ambao hautusaidii kabisa.
Labda nimalizie kwa kuwakumbusha Makocha wazalendo maamuzi yao waliyoyafanya hapo nyuma ambayo hayana tofauti sana na kile anachofanya Maximo kwa sasa.
S.Mziray: Kocha huyu wakati akiwa kocha mkuu wa timu ya taifa aliwahi kumuita kikosini mchezaji Magadula ambaye alikuwa hajawai kucheza super ligi hata mara moja.
Sunday Kayuni: Aliwahi kumuita kikosini mchezaji Nteze John Lungu ilhali machezaji huyu alikuwa akisotea benchi katika timumyake ya Simba.
Wito wangu kwenu nyote ni kuwa hatuisaidii timu ya taifa kwa kupiga kelele zisizo na msingi, tutambue ukweli tufanye kazi kulekebisha matatizo yaliyopo katika taifa. Sio lazima wote tuwe makocha wa timu ya Taifa, tunaweza kutoa mchango kwa Taifa kwa kulea vipaji hata katika maeneo tunayoishi.
Mbona sijaona kampeni za watu kumpongeza Maximo pale timu inapofanya vizuri? Ina maana toka apewe timu hajawahi kufanikiwa? au tunafumbia macho mafanikio na kuangalia matatizo?
Comments
Post a Comment