Ni wazi kuwa wapenzi wa timu ya Yanga ya Tanzania watakuwa wamesononeshwa sana na kufungwa kwa timu yao. Ni ukweli usipingika kuwa katika soka lolote laweza kutokea. Kwa upande wangu niliweza kuyaona haya machache.
Al Akhdar waliifanya home work yao vizuri. ni wazi kuwa walitumia vema mchezo uliochezwa kwao Libya kufanya Match analysis. Ninasema hivyo kutokana na jinsi walivyoweza kudhibiti uchezaji wa Yanga kama timu na ule wa mchezaji mmoja mmoja.
Kwa upande wa wachezaji ilionyesha wazi kuwa waliweza kutambua uchezaji wa wachezaji kama Mrisho Ngasa, Mourice Sunguti, na Abdi Kassim.
Nikitolea mfano wa Ngasa; ni wazi kuwa walijuwa vema kwamba Ngasa ni mchezaji mwenye speed na mwenye uwezo mkubwa wa kupiga chenga na kutoa pasi nzuri. Wao waliweza kutengeneza mfumo wa kumkaba Ngasa asiweze kufanya haya yote. Katika kumkaba Ngasa walitumia wachezaji wawili, mmoja akitangulia mbele kumzuia kwa karibu (committing) na wapili alikuwa aki support kwa nyuma. pindi Ngasa akifanikiwa kumpita huyu wa kwanza huyu wa pili anafiaka kwa haraka sana kuuondoa mpira ule(walifanikiwa katika hili kwa vile walikuwa wakiitumia vema ile concept ya kuwa wa kwanza kwenye mpira-Being first to the ball).
Katika hili la Ngasa kilichotakiwa kufanyika ni either Ngasa kwa vile ni mwepesi na ana mbio,kutumia uwezo wake wa kutoa na kupokea pasi. Alitakiwa asijaribu tena kupiga chenga bali kutoa pasi kwa haraka na kufungua tena ili apewe pasi tena. Hilo kama lingeshindikana angejaribu pia kuhamia upande wa pili,kutoka kulia kwenda kushoto na kujaribu mbinu zote mbili tena. Hili lingeshindikana Kocha angemtoa na kuingiza mtu mwingine mwenye mchezo tofauti na ule wa Ngasa.
Walijua pia kuwa Abdi Kassim ni mpigaji mzuri wa Mashuti hawakumpa nafasi Abdi kupiga mashuti mara kwa mara. Kushindwa kutumia vema mguu wa kulia ni jambo pia linalomkwamisha sana Abdi.
Pengo la Nsajigwa liliweza pia kuonekana kama ukiufananisha uchezaji wa Mbuna na Nsajigwa. Wote wana Nguvu na uwezo wa kupanda, lakini nsajigwa anasaidia sana katika mashambulizi kuliko Mbuna. nsajigwa huweza kutoa krosi nzuri ambazo mara nyingi zimekuwa zikitumiwa vema na wafungaji wa Yanga na hata wale wa timu ya taifa. Mbuna alikuwa na haraka na pasi zake nyingi kupotea.
Al Akhdari waliweza kutumia mipira mirefu ya pembeni hivyo kuwakwepa Yanga waliokuwa wengi kati kati na wachache pembeni nyuma. Hili linatokana na mfumo wanaotumia yanga hivyo kuwa na mapengo katika full backs.
Athman Idd alijitahidi kuleta uhai lakini anahitajika sana kufanyia mazoezi upigaji wa penetrating passes,Idd ameonekana mwenye control nzuri, nguvu na speed. Anapiga vizuri sana square passes lakini ana tatizo katika kutoa penetration(passes).
Al akdhar walijua wazi kuwa Yanga wana nguvu na hivyo kujitahidi sana kutopoteza nguvu yao katika kipindi cha kwanza.
Ninaweza kusema kilichowafunga yanga ni maandalizi na zaidi usomaji wa mchezo wao wa kwanza uliofanyika Libya. Ni wazi wenzao waliutumia vema kuliko yanga wenyewe.
Al Akhdar waliifanya home work yao vizuri. ni wazi kuwa walitumia vema mchezo uliochezwa kwao Libya kufanya Match analysis. Ninasema hivyo kutokana na jinsi walivyoweza kudhibiti uchezaji wa Yanga kama timu na ule wa mchezaji mmoja mmoja.
Kwa upande wa wachezaji ilionyesha wazi kuwa waliweza kutambua uchezaji wa wachezaji kama Mrisho Ngasa, Mourice Sunguti, na Abdi Kassim.
Nikitolea mfano wa Ngasa; ni wazi kuwa walijuwa vema kwamba Ngasa ni mchezaji mwenye speed na mwenye uwezo mkubwa wa kupiga chenga na kutoa pasi nzuri. Wao waliweza kutengeneza mfumo wa kumkaba Ngasa asiweze kufanya haya yote. Katika kumkaba Ngasa walitumia wachezaji wawili, mmoja akitangulia mbele kumzuia kwa karibu (committing) na wapili alikuwa aki support kwa nyuma. pindi Ngasa akifanikiwa kumpita huyu wa kwanza huyu wa pili anafiaka kwa haraka sana kuuondoa mpira ule(walifanikiwa katika hili kwa vile walikuwa wakiitumia vema ile concept ya kuwa wa kwanza kwenye mpira-Being first to the ball).
Katika hili la Ngasa kilichotakiwa kufanyika ni either Ngasa kwa vile ni mwepesi na ana mbio,kutumia uwezo wake wa kutoa na kupokea pasi. Alitakiwa asijaribu tena kupiga chenga bali kutoa pasi kwa haraka na kufungua tena ili apewe pasi tena. Hilo kama lingeshindikana angejaribu pia kuhamia upande wa pili,kutoka kulia kwenda kushoto na kujaribu mbinu zote mbili tena. Hili lingeshindikana Kocha angemtoa na kuingiza mtu mwingine mwenye mchezo tofauti na ule wa Ngasa.
Walijua pia kuwa Abdi Kassim ni mpigaji mzuri wa Mashuti hawakumpa nafasi Abdi kupiga mashuti mara kwa mara. Kushindwa kutumia vema mguu wa kulia ni jambo pia linalomkwamisha sana Abdi.
Pengo la Nsajigwa liliweza pia kuonekana kama ukiufananisha uchezaji wa Mbuna na Nsajigwa. Wote wana Nguvu na uwezo wa kupanda, lakini nsajigwa anasaidia sana katika mashambulizi kuliko Mbuna. nsajigwa huweza kutoa krosi nzuri ambazo mara nyingi zimekuwa zikitumiwa vema na wafungaji wa Yanga na hata wale wa timu ya taifa. Mbuna alikuwa na haraka na pasi zake nyingi kupotea.
Al Akhdari waliweza kutumia mipira mirefu ya pembeni hivyo kuwakwepa Yanga waliokuwa wengi kati kati na wachache pembeni nyuma. Hili linatokana na mfumo wanaotumia yanga hivyo kuwa na mapengo katika full backs.
Athman Idd alijitahidi kuleta uhai lakini anahitajika sana kufanyia mazoezi upigaji wa penetrating passes,Idd ameonekana mwenye control nzuri, nguvu na speed. Anapiga vizuri sana square passes lakini ana tatizo katika kutoa penetration(passes).
Al akdhar walijua wazi kuwa Yanga wana nguvu na hivyo kujitahidi sana kutopoteza nguvu yao katika kipindi cha kwanza.
Ninaweza kusema kilichowafunga yanga ni maandalizi na zaidi usomaji wa mchezo wao wa kwanza uliofanyika Libya. Ni wazi wenzao waliutumia vema kuliko yanga wenyewe.
Comments
Post a Comment