Habari ya kazi wapenzi wa mchezo huu wa soka. Leo hii ningependa kuandika kuhusiana na malengo ya mwalimu katika kufundisha, na namna ya ufundishaji ili kukidhi malengo hayo.
Mwalimu wa soka anayeiandaa timu yake kwa ajili ya mchezo uliyo mbele yake. Malengo yake yanaweza kuwa kushambulia zaidi au ulinzi zaidi.
Nitajaribu kuchambua malengo haya na kuangalia vitu mihimu vya kufundisha katika hali hizi mbili.
Iwapo lengo lako ni kushambulia (Attacking),basi itakubidi uazimie na kufundisha malengo haya matatu ya ushambuliaji;
Lengo la kwanza;
Andaa timu yako ili iweze kuingia katika eneo la adui (i.e the attacking third of the field. Kuna mbinu tano za kufuata ili uweze kufanikiwa katika hili;
1. Fundisha timu yako kutumia mipira mirefu itakayofika nyuma ya ngome(walinzi) wa timu pinzani.
2. Fundisha washambuliaji wako jinsi ya kukimbia mbele bila mpira (kwa lengo la kutafuta nafasi ya kupokea mpira na kufunga.
3. Wachezaji wako waweze kutoa pasi za uhakika,zinazoelekea mbele na zinazomfikia mwenzake (team mate)mguuni. Hakikisha kunakuwa na mchezaji wa kutoa msaada, kupokea pass na kutoa pasi kwenda mbele.
4. Fundisha jinsi ya kupokea pasi na kugeuka.
5. Fundisha jinsi ya kukimbia kwenda mbele wakiwa na mpira.
Lengo la Pili
Hakikisha timu yako ina maintain au ikiwezekana iongeze nguvu ya ushambuliaji pindi mapira ukiwa katika eneo la timu pinzani (third of the attacking field). Hapa pia kuna mabo matano ya kuzingatia na kufundisha.
1. Pindi nafasi inapopatikana wachezaji wapige mashuti golini.
2. Ikiwezekana washambuliaji wako washambulie huku waki-drible.
3. Inapowezekana pasi za wachezaji wako ziwe zinapita nyuma ya safu ya ulinzi ya timu pinzani.
4. Pindi nafasi inapopatikana mawinga wako wawe wepesi kupiga krosi zikazoweza kuwavuka walinzi wa timu pinzania.
5. Hakikisha team yako inaendelea kuwa compact.
Pindi timu yako itakapofanikiwa kutimiza lengo hilo la pili itafanya kazi ya kutimiza lengo la tatu kuwa rahisi zaidi.
Lengo la tatu
Hapa lengo letu ni timu iweze kufanya vizuri zaidi ya timu pinzani katika vitu muhimu vifuatazo;
1. Kupiga mashuti; Upigaji wa mashuti golini kila mara nafasi itokeapo huongeza nafasi zaidi za kupiga mashuti kwa mipira inayorudi toka goli la timu pinzani. Nafasi hizi hutokea aidha baada ya kungonga mwamba ama kuokolewa na walinzi au kipa.
2. Kupata nafasi za kupiga kona, kurusha mipira iliyotolewa na wapinzani, na mipira ya adhabu mbalimbali.
3. Nafasi za kupiga krosi
4. Uwezo wa kurudisha mipira inayopotelea katika eneo la adui (ukabaji katika eneo la ushambuliaji.
Kufikia hapo utakuwa umeweza kuinandaa timu yako iweze kucheza mchezo wa kushambulia. Kesho tutajitahidi kuangalia lengo likiwa ni kulinda zaidi (Defensive game)
Mwalimu wa soka anayeiandaa timu yake kwa ajili ya mchezo uliyo mbele yake. Malengo yake yanaweza kuwa kushambulia zaidi au ulinzi zaidi.
Nitajaribu kuchambua malengo haya na kuangalia vitu mihimu vya kufundisha katika hali hizi mbili.
Iwapo lengo lako ni kushambulia (Attacking),basi itakubidi uazimie na kufundisha malengo haya matatu ya ushambuliaji;
Lengo la kwanza;
Andaa timu yako ili iweze kuingia katika eneo la adui (i.e the attacking third of the field. Kuna mbinu tano za kufuata ili uweze kufanikiwa katika hili;
1. Fundisha timu yako kutumia mipira mirefu itakayofika nyuma ya ngome(walinzi) wa timu pinzani.
2. Fundisha washambuliaji wako jinsi ya kukimbia mbele bila mpira (kwa lengo la kutafuta nafasi ya kupokea mpira na kufunga.
3. Wachezaji wako waweze kutoa pasi za uhakika,zinazoelekea mbele na zinazomfikia mwenzake (team mate)mguuni. Hakikisha kunakuwa na mchezaji wa kutoa msaada, kupokea pass na kutoa pasi kwenda mbele.
4. Fundisha jinsi ya kupokea pasi na kugeuka.
5. Fundisha jinsi ya kukimbia kwenda mbele wakiwa na mpira.
Lengo la Pili
Hakikisha timu yako ina maintain au ikiwezekana iongeze nguvu ya ushambuliaji pindi mapira ukiwa katika eneo la timu pinzani (third of the attacking field). Hapa pia kuna mabo matano ya kuzingatia na kufundisha.
1. Pindi nafasi inapopatikana wachezaji wapige mashuti golini.
2. Ikiwezekana washambuliaji wako washambulie huku waki-drible.
3. Inapowezekana pasi za wachezaji wako ziwe zinapita nyuma ya safu ya ulinzi ya timu pinzani.
4. Pindi nafasi inapopatikana mawinga wako wawe wepesi kupiga krosi zikazoweza kuwavuka walinzi wa timu pinzania.
5. Hakikisha team yako inaendelea kuwa compact.
Pindi timu yako itakapofanikiwa kutimiza lengo hilo la pili itafanya kazi ya kutimiza lengo la tatu kuwa rahisi zaidi.
Lengo la tatu
Hapa lengo letu ni timu iweze kufanya vizuri zaidi ya timu pinzani katika vitu muhimu vifuatazo;
1. Kupiga mashuti; Upigaji wa mashuti golini kila mara nafasi itokeapo huongeza nafasi zaidi za kupiga mashuti kwa mipira inayorudi toka goli la timu pinzani. Nafasi hizi hutokea aidha baada ya kungonga mwamba ama kuokolewa na walinzi au kipa.
2. Kupata nafasi za kupiga kona, kurusha mipira iliyotolewa na wapinzani, na mipira ya adhabu mbalimbali.
3. Nafasi za kupiga krosi
4. Uwezo wa kurudisha mipira inayopotelea katika eneo la adui (ukabaji katika eneo la ushambuliaji.
Kufikia hapo utakuwa umeweza kuinandaa timu yako iweze kucheza mchezo wa kushambulia. Kesho tutajitahidi kuangalia lengo likiwa ni kulinda zaidi (Defensive game)
Comments
Post a Comment