Ni matumaini yangu kuwa leo pia tupo katika mwelekeo mmoja katika jitihada za kuufamu zaidi mchezo wetu wa soka.
Jana tuliongelea mikakati na malengo pindi unapohitaji kufundisha timu yako iweze kucheza mchezo wa kushambulia zaidi. Leo tutaangalia kwa ufupi ufundishaji pale unapohitaji kuzuia zaidi.
Njia bora zaidi ya ulinzi ni kuhakikisha timu yako inaweza kuzuia/kupokonya mipira mingi tokea katika eneo la timu pinzani. Wafundishe washambuliaji wako mbinu za ukabaji pia, ili waweze kuwa ndio mstari wa kwanza wa ulinzi kwa timu yako.
Itakuwa rahisi kwako kama timu yako itaendelea kuwa "compact". Kuwa Compact kutaisaidia timu yako kutekeleza mambo muhimu yafuatayo;
1. Hii inamaanisha kuwa itakuwa rahisi kwa timu yako kumkaba na kufanikiwa kumpokonya mpira mchezaji wa timu pinzani. Hii itamzuia au kusaidia kumchelewesha mpinzani kupeleka mpira mbele kwa washambuliaji wake.
2. Mchezaji wako (mshambuliaji) anayezuia mpira au kujaribu kumkaba mchezaji wa timu pinzani,atapata msaada wa ulinzi kutoka kwa mwenzake. PIa itasaidia kufanya marking, kuzuia nafasi (Cover space).
3. Itakuwa rahisi kwa wachezaji wako kuwakaba wachezaji wa timu pinzani wanaosonga mbele kushambulia.
Uwezekano wa timu yako kufungwa utapungua iwapo, wachezaji wako wanaolinda eneo linazozunguka eneo la penati watafanikiwa kutekeleza yafuatayo;
1. Iwapo watajitahidi kuwa wa kwanza kuufikia mpira
2. Kuokoa kwa kupiga mipira ya juu inayo kwenda mbali na yenye upana.
3. Waweze kuzuia eneo la "Far post".
4. Wahakikishe hawaponkonywi na timu pinzani haimiliki mpira katika eneo la ulinzi la timu yako. Wafundishe Kuziba nafasi, watawale eneo, wafanye "marking", waweze kufuatilia move zote za wapinzani ili kuwadhibiti
Jambo la kuzinga tia ni kwa walinzi wako kujaribu kukaa kama pembe tatu (napendelea zaidi kuiita umbo la sambusa" kuzingatia mahali mpira ulipo (iwapo upo kwa adui). Haya yafanyike kwa kuzingatia mahali ulipo mpira, mahali alipo mchezaji wa timu pinzani anayeweza kupatiwa pasi au aliyelengwa kupewa pasi, na usawa wa goli lenu.
Namna watavyojipanga ndiyo itakayo wasaidia kufanya vitu hivi vitatu;
1. Kama mpira utapigwa kwenda nyuma yao, wataweza kumzidi na kufika mapema mahali mpira ulipo kuliko adui aliye karibu.
2. Kama mpira utapelekwa kwa adui aliye karibu basi hii itawasaidia kuweza kujipanga wakati mpira ukiwa bado katika mwendo.
3. Watafanikiwa kuwa katika nafasi nzuri ya kuuona mwenendo wa mpira na wachezaji wa timu pinzani wakati wote wa mchezo.
Zaidi ya yote waandae wachezaji wako kisaikolojia ili waweze kuwa makini na kuzingatia hayo yote muda wote wa mchezo.
Jana tuliongelea mikakati na malengo pindi unapohitaji kufundisha timu yako iweze kucheza mchezo wa kushambulia zaidi. Leo tutaangalia kwa ufupi ufundishaji pale unapohitaji kuzuia zaidi.
Njia bora zaidi ya ulinzi ni kuhakikisha timu yako inaweza kuzuia/kupokonya mipira mingi tokea katika eneo la timu pinzani. Wafundishe washambuliaji wako mbinu za ukabaji pia, ili waweze kuwa ndio mstari wa kwanza wa ulinzi kwa timu yako.
Itakuwa rahisi kwako kama timu yako itaendelea kuwa "compact". Kuwa Compact kutaisaidia timu yako kutekeleza mambo muhimu yafuatayo;
1. Hii inamaanisha kuwa itakuwa rahisi kwa timu yako kumkaba na kufanikiwa kumpokonya mpira mchezaji wa timu pinzani. Hii itamzuia au kusaidia kumchelewesha mpinzani kupeleka mpira mbele kwa washambuliaji wake.
2. Mchezaji wako (mshambuliaji) anayezuia mpira au kujaribu kumkaba mchezaji wa timu pinzani,atapata msaada wa ulinzi kutoka kwa mwenzake. PIa itasaidia kufanya marking, kuzuia nafasi (Cover space).
3. Itakuwa rahisi kwa wachezaji wako kuwakaba wachezaji wa timu pinzani wanaosonga mbele kushambulia.
Uwezekano wa timu yako kufungwa utapungua iwapo, wachezaji wako wanaolinda eneo linazozunguka eneo la penati watafanikiwa kutekeleza yafuatayo;
1. Iwapo watajitahidi kuwa wa kwanza kuufikia mpira
2. Kuokoa kwa kupiga mipira ya juu inayo kwenda mbali na yenye upana.
3. Waweze kuzuia eneo la "Far post".
4. Wahakikishe hawaponkonywi na timu pinzani haimiliki mpira katika eneo la ulinzi la timu yako. Wafundishe Kuziba nafasi, watawale eneo, wafanye "marking", waweze kufuatilia move zote za wapinzani ili kuwadhibiti
Jambo la kuzinga tia ni kwa walinzi wako kujaribu kukaa kama pembe tatu (napendelea zaidi kuiita umbo la sambusa" kuzingatia mahali mpira ulipo (iwapo upo kwa adui). Haya yafanyike kwa kuzingatia mahali ulipo mpira, mahali alipo mchezaji wa timu pinzani anayeweza kupatiwa pasi au aliyelengwa kupewa pasi, na usawa wa goli lenu.
Namna watavyojipanga ndiyo itakayo wasaidia kufanya vitu hivi vitatu;
1. Kama mpira utapigwa kwenda nyuma yao, wataweza kumzidi na kufika mapema mahali mpira ulipo kuliko adui aliye karibu.
2. Kama mpira utapelekwa kwa adui aliye karibu basi hii itawasaidia kuweza kujipanga wakati mpira ukiwa bado katika mwendo.
3. Watafanikiwa kuwa katika nafasi nzuri ya kuuona mwenendo wa mpira na wachezaji wa timu pinzani wakati wote wa mchezo.
Zaidi ya yote waandae wachezaji wako kisaikolojia ili waweze kuwa makini na kuzingatia hayo yote muda wote wa mchezo.
Comments
Post a Comment